HAHAAAA WAKAKA WAMKAGUA MREMBO KAMA ANA HIPSI ZA KICHINA

 
Mwanamke mmoja jijini Nairobi amewaacha vinywa wazi wakazi  wengi wa jiji hilo baada ya kumshuhudia mwanadada mmoja mrembo sana akitaka kuchojoa nguo yake ili awe mtupu kwa lengo la kumthibitishia wananchi hao kuwa makalio na hipsi zake sio ya kichina wala hayasababishwi na chupi zenye sponji zenye kunenepesha maungo hayo kama wadada wengi wanavyopendelea.                                                               
Mkasa wa dada huyo kutaka kuuthibitishia Umma ulijiri baada ya kikundi fulani cha watu waliokuwa wakinong'ona na kuteta alipokatisha kijiweni kwao kwamba lazima mwanadada huyo anasaidiwa na chupi za sponji zenye kutengeneza umbo zuri hilo zuri na wala sio bure.
Dada huyo mrembo kupindukia na mwenye umbo matata alisimama ghafla na kuwaambia wakaka hao "samahani sana brothers sijawahi kutumianga hizo medicine za kichina,hili ni umbo langu originali ngoja nikuonyeshange" hapo ndipo bila kuwepo kwa baadhi ya watu wastaarabu wa kumsihi aachane na wakaka hao aendelee na safari zake,loo dada alikuwa anamwaga radhi bila hiyana.

0 comments: